April 25, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Cameroon's President Paul Biya is seen at the 72nd United Nations General Assembly at U.N. headquarters in New York City, U.S. September 22, 2017. REUTERS/Stephanie Keith - RC1A35221360

Wanajeshi waua raia, Serikali yakiri

Na Mwandishi Wetu

YAUNDE, Ofisi ya Rais wa Cameroon imekiri kuwa wanajeshi watatu walishirikiana na wanamgambo wenye silaha kuwaua raia 23 ikiwemo watoto 10 katika jimbo lenye wakazi wanaozumngumza Kiingerereza ndani ya Kijiji cha Ntumbo mwezi Februari, mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu iliyosomwa kupitia redio ya taifa ilieleza kuwa, wanajeshi watatu na wapiganaji wa kundi la waasi walivamia kambi moja ya jeshi na kuwaua watu hao kabla ya kuchoma moto eneo hilo kuficha ushahidi.

Awali, Serikali ya Cameroon iliyapinga madai ya kuhusika na mauaji hayo kwenye jimbo ambalo wapiganaji wanaotaka kujitenga kwa jamii ya wanaozungumza kiingereza wanapambana na vikosi vya Serikali kwa miaka miwili.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, mauaji hayo ya raia yalitokea usiku wa Februari 13 katika kijiji cha Ntumbo, Ambazonia.

Hapo kabla jeshi la Cameroon lilidai vifo vya watu hao vilitokana na ajali ya moto wakati wa mapambano na wanaotaka kujitenga.