April 29, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Ulenge atema cheche uhalifu mitandaoni katika Bunge la Dunia

Na Yusuph Mussa, TimezMajira Online

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Mhandisi Mwanaisha Ulenge ameutaka Umoja wa Mataifa (UN) uweke kipaumbele katika miundombonu ya kidigitali ambayo italinda mifumo dhidi ya mashambulizi na uhalifu wa mitandaoni

Mhandisi Ulenge amemwaga tena cheche hizo Machi 13, 2023 kwenye Kongamano la Umoja wa Mataifa katika Bunge la Dunia (IPU) linalofanyika nchini Bahrain wakati anajibu swali lililoulizwa na Umoja wa Mataifa kuwa, nini iwe ni kipaumbele wakati ujao kwenye Ulimwengu wa kidigitali?

Mhandisi Ulenge alijibu kwa kusema kwamba, wana sayansi wanasema vita vijavyo vinatajwa kuwa ni kati ya binadamu na teknolojia, na binadamu anataka kuitumia teknolojia kukua kiuchumi, lakini wakati huo huo, mashambulizi ya mtandaoni na uhalifu wa mitandaoni unamrudisha nyuma binadamu kukua kiuchumi.

“Wana sayansi wanasema vita vijavyo vinatajwa kuwa ni kati ya binadamu na teknolojia. Binadamu anataka kuitumia Teknolojia kukua kiuchumi wakati mashambulizi ya mtandaoni na uhalifu wa mitandaoni unamrudisha nyuma binadamu kukua kiuchumi.

“Hivyo Umoja wa Mataifa uweke kipaumbele katika miundombonu ya kidigitali ambayo italinda mifumo dhidi ya mashambulizi na uhalifu wa mitandaoni. Wanaofanya biashara ya kuuza savers za mitandao wanapaswa kujali ulindaji wa taarifa binafsi, na Tanzania imeshatunga Sheria ya ulindaji wa taarifa binafsi” alisema Mhandisi Ulenge

Mbunge wa Tanzania Mhandisi Mwanaisha Ulenge, akichangia kwenye Kongamano la Umoja wa Mataifa katika Bunge la Dunia (IPU) wakati anajibu swali lililoulizwa na Umoja wa Mataifa kuwa, nini iwe ni kimbaumbele wakati ujao kwenye Ulimwengu wa kidigitali?. (Picha na mtandao).
Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya Wabunge wa Tanzania kwenye Kongamano la Umoja wa Mataifa katika Bunge la Dunia (IPU) linalofanyika nchini Bahrain. Wengine ni Esther Matiko (kushoto), Mhandisi Mwanaisha Ulenge (kulia), Elibariki Kingu (wa pili kulia), na Faustine Ndugulile (katikati). (Picha na mtandao).
Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson na baadhi ya Wabunge wa Tanzania, ni miongoni mwa washiriki kwenye Kongamano la Umoja wa Mataifa katika Bunge la Dunia (IPU) linalofanyika nchini Bahrain. Yeye na Wabunge watano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, wanashiriki mkutano huo. (Picha na mtandao).