May 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Muonekano wa Kituo cha kuuza mafuta ya Petroli na Dizeli cha serikali (TANOIL)kitakachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC) kupitia Kampuni ya Mafuta ya TANOIL, kilichofunguliwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, Juni 06, 2020 wilayani Musoma mkoani Mara.

TPDC yarudi rasmi katika biashara ya mafuta nchini

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Mara

WAZIRI wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amezindua biashara ya Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) ya usambazaji wa mafuta ya petroli na dizeli pamoja na bidhaa zitokanazo na mafuta hayo.

Uzinduzi huo ulifanyika kwa Waziri Kalemani kuzindua pia vituo vya mafuta zaidi ya 10 nchini vinavyomilikiwa na TPDC ambavyo vitatoa huduma ya kuuza mafuta kwa wananchi chini ya usimamizi wa shirika hilo.

Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani akikata sili katika gari iliyobeba mafuta, ili kufungua koki kuruhusu mafuta kuingia katika matanki ya kuhifadhi mafuta ya kituo cha kuuza mafuta ya Petroli na Dizeli cha TANCOIL,alipozindua rasmi biashara ya mafuta katika kituo hicho kitakachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania( TPDC) kupitia Kampuni ya Mafuta ya TANCOIL, kilichofunguliwa na Waziri huyo , Juni 06, 2020 wilayani Musoma mkoani Mara.

Zoezi la uzinduzi wa vituo hivyo Kitaifa umefanyika mjini Musoma mkoani Mara alipozindua vituo viwili cha Musoma na Tarime vilivyopo mkoani hapa akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Subira Mgalu na watendaji wa wizara yake.

Amesema, mwezi huu wameanza na vituo saba na kwamba, vituo vyote nchini vitakuwa chini ya usimamizi wa TPDC huku akisema kuwa vituo vyote vinapaswa kusimamiwa vyema na kutoa huduma kwa ufanisi unaotakiwa kwa wananchi.

Amesema kuwa, kupitia uzinduzi wa vituo hivyo viwili vya Mkoa wa Mara vingine vyote vilizinduliwa rasmi nchini huku akisisitiza sera inataka kupeleka nishati vijijini.

Naibu Waziri wa Nishati , Subira Mgalu akizungumza na wakazi wa Mkoa wa Mara wakati wa ufunguzi wa kituo cha kuuza mafuta ya Dizeli na Petroli cha serikali kitakachosimamiwa na TPDC kupitia Kampuni ya Mafuta ya TANOIL, Dkt. Kalemani alifungua kituo hicho, Juni 06 ,2020, wilayani Musoma mkoani Mara.

Waziri Kalemani amesema,uzinduzi wa vituo hivyo ni hatua mojawapo ya kusogeza huduma za nishati karibu kwa wananchi ambao wanapaswa kunufaika na huduma hizo, kwa kuzitumia katika shughuli za kujiletea maendeleo kama ambavyo sera inaelekeza.

“Nishati siyo umeme peke yake, mafuta ni nishati, gesi ni nishati, upepo ni nishati, lakini tumeanza kupeleka nishati vijijini ni katika harakati za utekelezaji wa azima ya Serikali ya kufikisha huduma hizi za nishati kwa wananchi ziwasaidie kupiga hatua za kimaendeleo,”alisema.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said akizungumza na wakazi wa Mkoa wa Mara wakati wa ufunguzi wa kituo cha kuuza mafuta ya Dizeli na Petroli cha serikali kitakachosimamiwa na TPDC kupitia Kampuni ya Mafuta ya TANOIL, Dkt. Kalemani alifungua kituo hicho, Juni 06 ,2020, wilayani Musoma mkoani Mara.

Aliongeza kuwa, zoezi la usambazaji wa gesi asilia majumbani linakuja na kwamba utekelezaji wake unaanza mwakani, alisema wametoa maelekezo kwa wasambazaji wote wa gesi za mitungi bei ifanane isiwe kubwa, alisema wameunda timu ya kufuatilia na kufanya uratibu ili bei hiyo iwe ndogo isiwaumize wananachi.

Amesema,wataleta gesi ya kwenye mabomba ambayo bei yake itakuwa na punguzo la asilimia 40 na kwamba, haitakuwa na gharama kubwa ikilinganishwa na bei ya mkaa, hivyo akawataka wananchi kujiandaa kutumia nishati hiyo ambayo itakuwa rahisi na kila mmoja atamudu gharama ya matumizi yake.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima wakielezana jambo wakati wa ufunguzi wa kituo cha kuuza mafuta ya Dizeli na Petroli cha serikali(TANOIL) kitakachosimamiwa na TPDC, Dkt. Kalemani alifungua kituo hicho Juni 06, 2020, wilayani Musoma mkoani Mara.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Dkt.James Mataragio amesema kuwa, Serikali iliingia kwenye biashara hiyo kwa mfumo wa soko huria kwa kuunda kampuni tanzu na kwamba ilifanikiwa kununua na kujenga vituo mbalimbali nchini ikiwemo Kituo cha Makuyuni na Makumira mkoani Arusha, Segera na Muheza mkoani Tanga.

Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Waandamizi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake, Viongozi wa Serikali ya Mkoa wa Mara baada ya ufunguzi wa kituo cha kuuza mafuta ya Dizeli na Petroli cha serikali( TANOIL) kitakachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania( TPDC) kupitia Kampuni ya Mafuta ya TANCOIL, kilichofunguliwa na Waziri huyo , Juni 06, 2020 wilayani Musoma mkoani Mara.