Na Mwandishi wetu,Timesmajira
Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.Kellen-Rose Rwakatale amechukua rasmi fomu ya kugombea ubunge jimbo la Mlimba mkoani Morogoro.
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Rwakatale amesema anayo dhamira ya dhati kulitumikia jimbo hilo la Mlimba kwani anazijua changamoto zake.
Rwakatale ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shule za St Mary’s ndani na nje ya Tanzania amerejea maneno ya wazee ambao pia walimuita hivi karibuni kumtia moyo agombee amesema hana mashaka kwani amechukua fomu na kura zitaamua vema.


More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako