Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amemteua, Jaffar Mohamed Haniu kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu).
Kabla ya uteuzi huo,Haniu alikuwa Mtendaji Mkuu wa vyombo vya habari vya Africa Media Group Limited.Haniu anachukua nafasi ya Bw. Gerson Partinus Msigwa ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali. Uteuzi wa Bw. Haniu umeanza leo Juni 9, 2021.

More Stories
Tucta kuzindua kituo cha msaada kwa wafanyakazi wahamiaji Juni 11
Wanasiasa washauriwa kujikita kwenye masuala ya maendeleo
Watakiwa kuimarisha huduma za ushauri vyuoni