LONDON, England
KIUNGO wa timu ya Taifa ya England, Phil Foden huwenda
akaukosa mchezo wa fainali ya Kombe la Mataifa Ulaya
(Euro 2020)
dhidi ya Italia utakaochezwa leo jioni
kwenye Dimba la Wembley nchini Uingereza,baada ya
kupata jeraha la mguu.
Foden, mwenye umri wa miaka 21 alikuja kama mbadala wa
wachezaji watatu katika ushindi wa goli 2-1 dhidi ya
Denmark Jumatano jioni hatua ya nusu fainali,
lakini
mchezaji huyo alimumia mguu.
Kwa mujibu wa BBC Sport, inaripoti kwamba Foden
alionekana kutofanya
Mazoezi ya mwisho kabla ya Fainali
ya Mashindano ya Uropa, na sasa inaonekana kuwa
mashakani kucheza fainali hiyo leo.
Kocha wa timu ya Taifa ya England, Gareth Southgate
amekiri kwamba
wataalamu wa matibabu watalazimika
‘kutathmini’kuona ikiwa anaweza kucheza au hatashindwa.
Ana jeraha la mguu,Lakini italazimika kutathmini hilo
baadaye.
More Stories
Magwiji 27 wafuzu raundi ya tatu mashindano ya kumuenzi Lina
Mafanikio Wizara ya Ulinzi kwenye michezo miaka 60 ya muungano
Mbunge Bonnah agawa jezi za mashindano ya Bonah Cup 2024