Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Theobald Sabi amesema NBC inaendelea kukuza mshikamano na maelewano katika familia na jumuiya kupitia ibada ya iftari.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya Iftar kwa wateja wa NBC wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sabi amesema benki ya NBC imeamua kufanya tukio hili kwa ajili ya kukuza mshikamano na maelewano katika familia na jumuiya.
Sabi amesema, “tunaamini kufunga ni mafunzo, yanaleta maisha ya ukarimu, uchamungu, ukweli, furaha na mshikamano baina ya jamii,”

“Tunawashukuru wateja wetu kwa kuitikia wito na kuwa pamoja nasi katika hafla hii muhimu ya Iftar kwa ajili ya kurudisha kwa mwenyezi mungu kupitia ibada ya upendo, kutoa zaka na sadaka,”amesema
Aidha, Sabi ameendelea kuhamasisha watu binafsi na taasisi kuendelea kuwasaidia watu wengine kupitia ibada mbalimbali.

More Stories
Ndoto zilizovunjika: Jinsi Mimba za utotoni zinavyowakatisha Wasichana elimu nchini Rwanda,Tanzania na Sudan Kusini
Miaka 50 ya Sabasaba Vodacom yadhihirisha kuchochea mageuzi ya kidigital nchini
Milioni 750 kukamilisha kituo cha afya