Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Dar es Salaam
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetabiri uwezekano wa kunyesha mvua kubwa katika mikoa minane ya Tanzania ambazo zinaweza kusababisha mafuriko mkatika baadhi ya maeneo.
Mikoa hiyo ni Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe.
Akizungumza jana mchambuzi wa TMA, Joyce Makwata amesema mvua hizo zinatarajiwa kunyesha ndani ya saa 24 katika mikoa hiyo ambapo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari.
Makwata amesema mvua hizo zitasababisha baadhi ya makazi ya watu kuzungukwa na maji na barabara kutopitika.
Amesema wananchi wa maeneo hayo wanatakiwa kuchukua hatua hasa wale wanaoishi mabondeni na wafuatilie mara kwa mara taarifa za TMA.
More Stories
NMB ‘yafunga ndoa’ na wanawake wanaomiliki shule, vyuo Tanzania
RC Mwanza afanya ziara ya kikazi katika mradi wa uwekezaji jengo la Hotel ya nyota tano wa NSSF
Wasichana vinara waiomba serikali kuondoa kodi kwenye taulo za kike