April 27, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Moja ya mashindano ya tenis katika uwanja wa Wembledon.

Michuano ya Wimbledon sasa kufanyika 2021

LONDON, England

KWA mara ya kwanza tangu vita ya pili ya dunia, mashindano ya 134 ya mchezo wa Tenisi ya Wimbledon yameahirishwa hadi mwakani kutokana na janga la Virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid-19).

Awali mashindano hayo yalitakiwa kuchezwa kati ya Juni 29 hadi Julai 12 mwaka huu lakini sasa yatalazimika kuchezwa kuanzia Juni 28 hadi Julai 11 mwakani.

Mashindano hayo sasa yanaingia katika orodha ya mashindano makubwa yaliyoahirishwa hivi karibuni ikiwemo yale ya Euro 2020 na mashindano ya Olimpiki ya Tokyo, 2020 kutokana na hofu ya washiriki wake kupata maambukizi ya ugonjwa huo.

Pia mashindano makubwa ya French Open yaliyokuwa yamepangwa kuanza mwezi Mei, yameahirishwa hadi Septemba 20 mwaka huu endapo maambukizi hayo yatapungua na hali kuwa shwari.

Uingereza ambayo nchi nzima ipo chini ya uangalizi, klabu zote za mchezo huo zilitangaza uamuzi wake wa kumaliza mashindano ya wiki mbili ya tenisi kitu ambacho hakijafanyika kwenye hafla ya zamani ya mchezo wa ‘Grand Slam’ katika miaka 75.

“Hili ni jambo zito sana katika akili zetu kwani tukio pekee lililosimamisha mashindano lilikuwa ni Vita vya Dunia, lakini kufuatia kuzingatia kwa undani na kwa hali zote, tunaamini kwamba ni shida hii inayoikumba dunia itamalizika na uamuzi wa kusitisha mashindano haya kwa mwaka huu ni sahihi na badala yake tunaweza kutumia rasilimali zilizopaswa kutumika katika mashindano haya kusaidia jamii iliyoathirika na ugonjwa huu, ” alisema Mwenyekiti wa klabu, Ian Hewitt.

Bingwa mara nane wa taji hilo la Wimbledon, Roger Federer alizungumza kwa wachezaji wengi wa tenisi, maofisa na mashabiki na ujumbe wa neno moja kwenye mtandao wake wa Twitter aliloandika “Devastated” lakini wadau mbalimbali wakidai kuwa hiyo ni hatua nzuri kwake ya kujiweka sawa kuelekea mashindano Grand Slam kwani anatarajia kuwa hadi Agosti atakuwa amepona kutokana na upasuaji wa goti aliofanyiwa.

Pia ATP na WTA ilitangaza kwamba safari za kitaalam za wanaume na wanawake zitasimamishwa hadi angalau Julai 13, na kuleta idadi ya mashindano ya tenisi ya wasomi walioathirika na corona tangu Machi huku pia wameahirisha ziara za ITF World Tour iliyokuwa ifanyike wiki mbili za mwanzo za mwezi Julai.

Mashindano ya Wimbledon ya kwanza yalifanyika mwaka 1877 na yamekuwa yakifanyika kila mwaka isipokuwa 1915-18 kwa sababu ya Vita vya Kwanza vya Dunia, na mwaka 1940-45 kwa sababu ya Vita pili ya Dunia.

Muda mfupi baada ya taarifa hiyo ya kuahitishwa kwa mashindano ya Wimbledon, Chama cha Tenisi cha Amerika kilitoa taarifa iliyosema kuwa, bado wana mpango wa kuwa mwenyeji wa michuano ya U.S. Open kama ilivyopangwa  kuanza Agosti 31 hadi Septemba 13 katika mji wa New York.

Kama ilivyo sasa, mashindano ya French Open yamepangwa kuanza siku sita baada ya kumalizika kwa mashindano ya wanaume huko Flushing Meadows, ambako katika  chumba cha mazoezi kimegeuzwa kuwa hospitali ya muda yenye vitanda 350 na Uwanja wa Louis Armstrong kwa sasa unatumika kuandaa vifurushi 25,000 vya chakula 25,000 kwa siku kwa wagonjwa, wafanyikazi, wanaojitolea na watoto wa shule katika mji.