Na Patrick Mabula, Kahama.
SERIKALI wilayani Kahama imesema inafanya uchunguzi juu ya tukio la miili ya watu wanne waliouawa kisha kutupwa katika mto uliopo kijiji cha Mwabomba kata ya Idahina halmashauri ya Ushetu na kukutwa ikiwa imeharibika vibaya ili sheria ichukue mkondo wake.
Mkuu wa wilaya ya Kahama , Anamringi Macha alisema miili ya watu hao waliouawa na watu wasiojulikana ilibainika jumapili iliyopita katika mto huo uliopo karibu na machimbo ya dhahabu ya Mwabomba ikiwa imeharibika vibaya huku sura zao kutotambulika .
Macha alisema serikali kwa kutumia vyombo vyake vya dola inafanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini watu waliofanya kitendo cha mauaji hayo na kuitupa miili hiyo katika mto huo unaotenganisha wilaya ya Kahama na wilaya ya Mbogwe mkoa wa Geita waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

More Stories
Mpogolo aagiza mitaro Kariakoo kuzibuliwa
TCRA, Polisi na mkakati wa kudhibiti uhalifu mtandaoni Rukwa
Tuzo shindani kuongeza tija ya sekta ya Maziwa