April 18, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mgombea Ubunge Jimbo la Ilemela kupitia CCM Dkt.Angeline Mabula akizungumza na wananchi alipokuwa akiomba kura.

Mabula adhamiria kuboresha miundombinu ya barabara Ilemela

Na Judith Ferdinand,Mwanza

IMEELEZWA kuwa kukosekana kwa miundombinu bora huchangia ukosefu wa maendeleo ambapo kipindi cha awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais John Magufuli kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt.Angeline Mabula wamefanikiwa kujenga barabara katika Kata ya Buswelu na bado wanaendelea.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wananchi wa Kata ya Buswelu uliofanyika uwanja wa shule ya msingi Buswelu katani hapo mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Ilemela DKt.Angeline Mabula,amesema wakati wanaingia madarakani mwaka 2015 kata hiyo ilikuwa haina barabara yenye lami.

Mgombea Ubunge Jimbo la Ilemela kupitia CCM Dkt.Angeline Mabula akizungumza katika mkutano wa kampeni wa chama hicho wa kuomba kura kwa wananchi uliofanyika uwanja wa Nyakato Sokoni Kata ya Nyakato Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza. Picha na Judith Ferdinand

Lakini ndani ya miaka mitano wamefanikiwa kujenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Nyakato Steel hadi Tx-Igombe yenye urefu wa km18.2 ambayo imeisha jengwa takribani km 5 anaimani inakwenda kukamilika ndani ya kipindi cha Dkt.John Magufuli endapo watachagua wagombea kwa ngazi zote wanaotokana na CCM.

Amesema,barabara yenye urefu wa km 9.2 kutoka Sabasaba kupita kiseke kuja Buswelu ambayo imewekewa na taa za barabarani zinazisaidia watu kufanya biashara mpaka usiku bila shida yoyote inekamilika.

“Kama hiyo haitoshi kuna barabara ya Busanda-Cocacola zaidi ya kilomita 3.38 ambayo nayo inaenda kujengea,tayari fedha zimetengwa za ujenzi wa barabara ya Buswelu-Kiseke Buyombe hivyo tuchagueni sisi wagombea wa CCM ili tutwende tukatekeleze na kukamilisha haya,” amesema Dkt.Angeline.

Pia amesema,kulikuwa na changamoto kubwa ya vivuko Kigala na Lagos zaidi ya milioni 112.2 tayari zimejenga madaraja hayo kwa ajili ya kuvukia na sasa hakuna changamoto hiyo,wanaenda kujengewa kituo cha afya katika kata hiyo huku zahanati ya Nyerere inaendelea kuboreshwa zaidi ili iendane na hadhi ya Baba wa taifa.

Mgombea Ubunge Jimbo la Ilemela kupitia CCM Dkt.Angeline Mabula akimnadi mgombea Udiwani wa Kata ya Kitangiri kupitia CCM Donald Protas kwenye mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wananchi wa mtaa wa Mahina Kata ya Kitangiri,uliofanyika kwenye uwanja wa mahina. Picha na Judith Ferdinand

Hata hivyo amesema suala la umeme katika jimbo hilo ulikua unapatikana kwa asilimia 35 sasa ni 75 bado 25 ambapo zaidi ya bilioni 1 zimetengwa kwa ajili ya kumalizia maeneo ambayo hayajapata umeme ikiwemo kata ya Buswelu pia katika sekta ya elimu wamejenga madarasa na madawati.