Na Penina Malundo, TimesMajira Online
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, ametangaza kifo cha Naibu Kamishna wa Polisi, Dhahiri Kidavashari kilichotokea leo katika Hospitali ya Christian Medical Center Trust (DCMCT) iliyopo, Dodoma ambako alikuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa taarifa ya IGP Sirro, Kamanda Dhahiri Kidavashari, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne Novemba, 17, 2020 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali hiyo.
Aidha IGP Sirro, amesema kuwa msiba upo Kisasa,Nyumba mia tatu jijini hapo huku taratibu za mazishi zikiwa zinaendelea.
More Stories
TPA yatekeleza agizo la Samia korosho kupitia Bandari Mtwara
Mvutano vyama vya wafanyakazi kikwazo vikao baraza la wafanyakazi Wizara ya ardhi
NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika jijini Arusha