October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Dkt.Ndugulile achaguliwa kuwa Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika

Dkt. Faustine Ndugulile, amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika katika uchaguzi uliofanyika leo Jumanne, tarehe 27 Agosti 2024 mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo. Dkt. Ndugulile amewashinda wagombea wengine watatu kutoka Senegal, Niger na Rwanda.