Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online, Zanzibar
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Othman Masoud Othman,Agosti 27, 2024 amejumuika pamoja na Viongozi Wakuu, Masheikh, na Waumini mbalimbali wa Kiislamu, katika Maziko ya Marehemu Mvita Mussa Kibendera.
Marehemu Mvita,alifariki Dunia usiku wa kuamkia Agosti 27,2024,ambaye ni Mama wa Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Dokta Saada Mkuya Salum,amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Sala imeongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi, Msikiti wa Ijumaa Mwembeshauri,na amezikwa katika Makaburi ya Mwanakwerekwe, Mkoa wa Mjini-Magharibi, Unguja.
Viongozi mbalimbali wa Serikali, dini, vyama vya siasa na jamii, wamehudhuria maziko hayo wakiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dokta Hussein Ali Mwinyi




More Stories
Utafiti wafichua mazito sekta ya uvuvi baharini
Takwimu Rasmi kuongoza utekelezaji Dira 2050
TBS kuadhimisha miaka 50,kuzindua kitabu chake