May 17, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Dkt. Mpango aelekea  nchini Ethiopia kumuwakilisha Rais Samia

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango leo tarehe 4 Februari 2022 ameondoka nchini kuelekea Addis Ababa  nchini Ethiopia kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 35 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) unaotarajiwa kufanyika tarehe 5 na 6 Februari 2022.