Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Historia imeandikwa Tanzania, baada ya Mkanda mwingine kubakia katika Ardhi ya Tanzania ambapo Bondia Said Mohamed maarufu kama Said Chino kuwa bingwa mpya wa IBA Intercontinental Championship kwa kumchapa mpinzani wake raia wa Afrika Kusini Lusanda Komanisa kwa pointi.
Said Chino ameshinda pambani hilo kwa point kutoka kwa majaji wote watatu
Kwa ushindi huo Said Mohamed amezwadia #KnockoutyaMama ya Shilingi milioni tano kama zawadi , ambapo katibu mkuu wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema kuwa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ameamua kuisapoti sekta yote ya michezo na kwasasa mapambano yote ya kimataifa yatakayohusisha mabondia wa Kitanzania basi Mh. Rais Samia atakuwa motisha kwa mabondia hao
KnockoutyaMAMA




More Stories
Watanzania zaidi ya 90 wanufaika ‘ ikiingia tu goli’
Yas yazindua msimu wa sita Zanzibar Marathon 2026
Tamasha kuhamasisha mapambano dhidi dawaza za kulevya lafana