Na Penina Malundo, TimesMajira Online, Dar es Salaam
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema ), kimeanza rasmi ratiba ya shughuli ya uchukuaji, kutafuta wadhamini na kurejesha fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania , Urais wa Zanzibar, Ubunge wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania na Uwakilishi wa Baraza la wawakilishi Zanzibar leo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo imesema watia nia nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watachukua fomu zao za kugombea Ofisi za Makao Makuu ya Chama, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Imesema kwa watia nia wa Urais wa Zanzibar, watachukua fomu zao Makao Makuu ya Chama, Kisiwandui, Unguja, Zanzibar.
“Kuanzia saa nne tunaanza utoaji wa fomu nanwapo baafhi ya watia nia wanaokuja kuchukua fomu ,”imesema
Aidha Katibu Mkuu wa Chama, John Mnyika atakuwa na kikao na watia nia wa ubunge na udiwani wa Kanda ya Pwani, itakayofanyika Hoteli ya Lions, Sinza, jijini Dar es Salaam.
More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo