Na Penina Malundo, TimesMajira Online, Dar es Salaam
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema ), kimeanza rasmi ratiba ya shughuli ya uchukuaji, kutafuta wadhamini na kurejesha fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania , Urais wa Zanzibar, Ubunge wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania na Uwakilishi wa Baraza la wawakilishi Zanzibar leo.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo imesema watia nia nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watachukua fomu zao za kugombea Ofisi za Makao Makuu ya Chama, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Imesema kwa watia nia wa Urais wa Zanzibar, watachukua fomu zao Makao Makuu ya Chama, Kisiwandui, Unguja, Zanzibar.
“Kuanzia saa nne tunaanza utoaji wa fomu nanwapo baafhi ya watia nia wanaokuja kuchukua fomu ,”imesema
Aidha Katibu Mkuu wa Chama, John Mnyika atakuwa na kikao na watia nia wa ubunge na udiwani wa Kanda ya Pwani, itakayofanyika Hoteli ya Lions, Sinza, jijini Dar es Salaam.
More Stories
Afisa Mtendaji Wazo huru achangia madawati 20 shule ya msingi Kiomboi-Bomani
Absa Dar City waunga mkono juhudi za Serikali uboreshaji Afya
Ndejembi atoa onyo kwa waajiri wasiowasilisha michango ya wafanyakazi wao NSSF