Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
BODI ya Sukari nchini Tanzania imesema msimamo wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuwalinda wananchi, wakulima, wawekezaji na wadau wengine muhimu kwa kuhakikisha inafanya maboresho makubwa kwa maslahi ya Watanzanaia wote.
Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania Profesa Kenneth Bengesi, aliwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku chache baada ya kupitishwa sheria mpya ya sukari nchini.
“Tunaendeleza majadiliano na wadau ili kutatua changamoto zote sambamba na kuikuza sekta ya sukari kwa sababu ni jambo nyeti na muhimu, hivyo tunalichukulia hili kwa umakini,”Alisema Profesa Bengesi.

Kwa siku za karibuni kumekuwa na mijadala kadhaa kutokana na siku chache zilizopita kugubikwa na uhaba wa sukari hali iliyoibua hofu kwa Watanzania wote.

More Stories
2030 Tanzania kifikia megawati 8,000 na megewati 70,000 ifikapo 2050
Msimu wa ununuzi wa ufuta Songwe ni Mei, miundo mbinu yaboreshwa
Tanzania yapiga hatua kibwa sekta ya Nishati