Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Ujumbe kutoka Benki ya NMB ukiongozwa na Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa Serikali na Ofisi ya Makao Makuu Ndogo ya Dodoma, Bi. Vicky Bishubo kwa nyakati tofauti umemtembelea Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Uratibu na Bunge, Dkt. Jim Yonazi pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Anderson Mutatembwa na kufanya mazungumzo ambayo yanalenga kuimarisha uhusiano kati ya Benki ya NMB na Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Uratibu na Bunge.
Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Waziri Mkuu – Sera, Uratibu na Bunge zilizopo Jijini Dodoma.
More Stories
RC Mwanza afanya ziara ya kikazi katika mradi wa uwekezaji jengo la Hotel ya nyota tano wa NSSF
Wasichana vinara waiomba serikali kuondoa kodi kwenye taulo za kike
Tigo watoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Karatu