Na Penina Malundo Timesmajira Online
CHAMA cha Mapindunzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, kimeongoza kwa wanachama wengi kumdhamini Rais John Magufuli katika kuwania nafasi ya Urais kwa awamu nyingine kwa kupitia Chama hicho.
Mwenyekiti CCM Mkoa, Innocent Kalogeris amewasilisha takribani Fomu za Wanachama 117,080 kumdhamini Rais leo Mkoani Dodoma alipokuwa akirudisha fomu za kugombea.
Mbali na wadhamini hao waliojitokeza kumdhani Rais Magufuli, pia Mwenyekiti huyo amekabidhi pesa zilizochangwa na wana CCM Mkoa huo, kiasi cha Sh. milioni moja kwa ajili ya kumpa Rais Magufuli.
More Stories
Lushanga mbaroni tuhuma za kusababisha ajali
Mwanafunzi SAUT afa maji Ziwa Victoria
Dkt.Tulia awezesha vijana 20 Jijini Mbeya kupata ajira kupitia mafunzo ya Uanagenzi