Na Mwandishi Wetu. Timesmajira
Timu ya Taifa ya Morocco, imekuwa nchi ya kwanza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) za 2023, zitakazofanyika nchini Ivory Cost mwaka huu.
Inchi hiyo ilikata tiketi ya kucheza michuano hiyo jana baada ya Afrika Kusini na Liberia kupata sare ya magoli 2-2.
Morocco inaongoza Kundi K, ikiwa na alama sita baada ya kushinda mechi mbili dhidi ya Liberia na Afrika Kusini.
Zimbabwe, ambayo awali ilipangwa Kundi K, iliondolewa na FIFA kucheza mechi za kufuzu AFCON kutokana na serikali ya Zimbabwe kuingilia masuala ya ligi ya soka ya nchi hiyo.

More Stories
Kamati ya Bunge Yapokea Taarifa ya AFCON 2027
Yanga yatwaa Ngao ya Jamii ,Simba chali
Wajinyakulia zawadi Kampeni ya ‘Vuna na Mixx’