Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MSANII wa kike anayefanya vizuri katika kiwanda cha Bongo fleva Faustine Charles maarufu ‘Nandy’, ameusifia wimbo wake ‘Nimekuzoea’ baada ya kufanya vyema katika mtandao wa Shazzam wiki hii.
Akitoa sifa hizo kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram Nandy amesema, amefarijika sana baada ya kuona wimbo huo umeshika nambari moja Afrika Mashariki.
“Nimekutana na playlist ya ngoma zilizotafutwa zaidi kwenye mtandao wa Shazzam kwa wiki hii Afrika mashariki, kwa mujibu wa Apple music, na Nimekuzoea imeshika namba 1 hapo!,” amesema Nandy.
More Stories
Twanga Pepeta waikubali ‘Speed’ ya Rais Samia
Ali Kiba aitaka jamii kuwasaidia watoto wenye uhitaji maalumu
Azam TV yazindua filamu mpya