Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MFANYABIASHAARA na Mzazi mwenza wa staa wa Bongofleva
na bosi wa Wasafi Media, Diamond Platnumz, Zarina
Hassan maarufu kama ‘Zari the boss lady’ameamua
kumpiga chini mpenzi wake maarufu kwa jina la King bae
2 au Dark Stallion, baada ya kuona hana manufaa naye.
Zari ambaye anaishi Afrika Kusini pamoja na watoto
wawili wa Mondi, aliandika ujumbe kwenye insta story
yake,kuwa mwanaume huyo inabidi amuache kwani hana
faida yoyote kwake.
“Nimemmisi, lakini inanibidi nimuache aondoke. Kwa
sababu kama hanijengi, hana faida kwangu siwezi
kuendelea naye,” ameandika Zari
Kufuatia hali hiyo baadhi ya mashabiki wamedai kuwa
hii inaweza kuwa muda muafaka kwa Mondi kurudisha
majeshi kwa Zari baada ya Dark Stallion ambaye alikuwa
raia wa Nigeria kutimuliwa.
More Stories
Tamasha la utamaduni mkoani Ruvuma lapamba moto, Rais Samia mgeni rasmi
TANAPA yazindua Twenzetu Kilele msimu wa nne
Shamrashamra maadhimisho ya miaka 60 JWTZ yaendelea