Na Penina Malundo, TimesMajira Online
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, ametangaza kifo cha Naibu Kamishna wa Polisi, Dhahiri Kidavashari kilichotokea leo katika Hospitali ya Christian Medical Center Trust (DCMCT) iliyopo, Dodoma ambako alikuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa taarifa ya IGP Sirro, Kamanda Dhahiri Kidavashari, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne Novemba, 17, 2020 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali hiyo.
Aidha IGP Sirro, amesema kuwa msiba upo Kisasa,Nyumba mia tatu jijini hapo huku taratibu za mazishi zikiwa zinaendelea.
More Stories
NMB ‘yafunga ndoa’ na wanawake wanaomiliki shule, vyuo Tanzania
RC Mwanza afanya ziara ya kikazi katika mradi wa uwekezaji jengo la Hotel ya nyota tano wa NSSF
Wasichana vinara waiomba serikali kuondoa kodi kwenye taulo za kike