Na Mwandishi Wetu
DUBAI, Wizara ya Mambo ya Masuala ya Waislamu na Miongozo katika Umoja wa Falme za Kiarabu imetangaza kusitishwa kwa sala za Taraweeh wakati wa mfungo wa Ramadan na badala yake zitafanyika nyumbani.
Hatua inayochukuliwa ikiwa pia sala katika misikiti imezuiwa hadi pale ambapo virusi vya corona (COVID-19) vitadhibitiwa.
Gazeti la Al Riyadh limemnukuu Waziri wa wizara hiyo, Dkt. Abdul Latif Al Sheikh akisema, “kusimamishwa kwa sala tano za kila siku katika misikiti ni muhimu zaidi kuliko kusimamishwa kwa sala za Taraweeh. Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu akubali maombi ya Taraweeh iwe imefanyika katika misikiti au nyumbani, jambo ambalo tunadhani ni bora kwa afya ya watu.
“Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu akubali maombi kutoka kwetu sisi sote na kulinda ubinadamu wetu kutokana na janga hili ambalo linasumbua ulimwenguni kote,”amefafanua Dkt.Al Sheikh.
Kwa kina jisomee katika gazeti la Majira…
More Stories
The Desk and Chair yatoa vifaa saidizi kwa Masatu na mkewe
jengo la mama,mtoto la bilioni 6.5 lazinduliwa Mbulu
Dkt.Malasusa ataka hospitali ya Haydom kuombea wafadhili wanaoishika mkono