LONDON, England
MKALI wa muziki kutoka nchini Nigeria, Wizkid
ameutaarifu umma kuwa tiketi ambazo zitatumika
katika shoo yake inayotarajiwa kufanyika nchini
Uingereza Novemba 28 mwaka huu zimemalizika mapema.
Nyota huyo amethibitisha Taarifa hizo za kumaliza
kwa tiketi za show yake kupitia kwenye Ukurasa wake
wa Instagram ambapo ameandika…….”Sold out the O2 in
12mins!! Love u london!!,” amesema Wizkid
Miongoni mwa nyimbo zake zinazofanya vizuri kwasasa
kwenye charts mbalimbali ni huu uitwao ‘Essence’
aliyomshirikisha Tems ambao kupitia mtandao wa
Youtube umetazamwa na watu zaidi ya 19,206,422.
More Stories
GETHSEMANE GROUP KINONDONI yaja na wimbo wa siku yetu kwaajili ya harusi
Startimes yazindua makala ya China, Africa
Mwanasheria wa Katavi aliyetimkia kwenye muziki achaguliwa tuzo za MIEMMA