LONDON, England
MKALI wa muziki kutoka nchini Nigeria, Wizkid
ameutaarifu umma kuwa tiketi ambazo zitatumika
katika shoo yake inayotarajiwa kufanyika nchini
Uingereza Novemba 28 mwaka huu zimemalizika mapema.
Nyota huyo amethibitisha Taarifa hizo za kumaliza
kwa tiketi za show yake kupitia kwenye Ukurasa wake
wa Instagram ambapo ameandika…….”Sold out the O2 in
12mins!! Love u london!!,” amesema Wizkid
Miongoni mwa nyimbo zake zinazofanya vizuri kwasasa
kwenye charts mbalimbali ni huu uitwao ‘Essence’
aliyomshirikisha Tems ambao kupitia mtandao wa
Youtube umetazamwa na watu zaidi ya 19,206,422.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”