Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye ameliagiza Jeshi la Polisi kutoa taarifa za matukio yote ya ajali za barabarani kwenye misafara ya viongozi nchini ambayo yanachukua maisha ya wana tasnia hiyo ili zipitiwe na kujua ni kwanini zinawagusa wanahabari ili kuchukua hatua ya kuweka itifaki nzuri itakayowalinda wanahabari wanapotimiza wajibu wao kwenye misafara ya viongozi.
Amesema hayo wakati akitoa pole kwenye hafla ya kuaga miili ya wanahabari watanoiliyofanyika mkoani Mwanza.
“Nilipokuwa nakuja huku wakubwa wangu wamenielekeza kuwa nifuatilie hili la ajali kwenye misafara ya viongozi,kwani waathirika wamekuwa ni waandishi wa habari,lazima tujue chanzo ni nini,”amesema.
Waziri Nape amesema jambo hilo watalisimamia kuhakikisha kuwa waandishi wa habari wote wanakuwa salama kwenye kutimiza majukumu yao.

Aidha alimaliza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha ya marehemu hao watano na amewasihi watu wote waendelee kuwakumbuka kwa kazi zao walizokuwa wakizifanya.
More Stories
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka