
Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online. Chalinze
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amekutana na kufanya mkutano na Madiwani na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze, wakiwemo Watendaji Kata, Maafisa Tarafa, Wakuu wa Idara za Halmashauri ya Chalinze na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Ramadhani Possy.

Kikao hicho kimetoa nafasi ya kujadili kwa pamoja majukumu na mipango ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 ambayo itawezesha Halmashauri ya Chalinze kutoa mchango wake mkubwa katika ustawi wa Taifa kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa.

More Stories
Kampuni ya Oryx Gas yakabidhi mitumgi 600 kwa wajasiriamali
DCEA yafanikiwa kuteketeza ekari 291.2 Mara
Manyire waanza ujenzi Sekondari mpya