May 18, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

TMDA yawanoa wadhibi wa vifaa tiba barani Afrika

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba Nchini (TMDA) inaendesha mafunzo ya siku tatu Jijini Dar es Salaam ya kufanya tathmini ya udhibiti wa vifaa tiba vya Wamama, Watoto wachanga na Watoto kwa wataalam wa vifaa tiba kutoka Mamlaka za udhibiti za nchi 11 za Afrika.

Kongamano hilo ni la kwanza Barani Afrika ambapo mafunzo hayo yanafanyika kufuatia nchi za Afrika kutokuwa na uwezo wa kudhibiti bidhaa za Wakinamama na Watoto hivyo mafunzo hayo yatasaidia uwezo wa kutathimini bidhaa kabla hazijaingia kwenye soko.

Kongamano hilo la siku tatu, limezinduliwa mapema leo na Mkurugenzi wa Vifaa tiba na vitendanishi Bi. Kissa Mwamwitwa aliyekuwa amemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Bw. Adam Fimbo ambapo ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya kwa kuipa uwezo TMDA kujulikana Afrika na kuweza kutoa utaalamu ambao wanatoa kwa Nchi zingine.

“Warsha hii imedhaminiwa na Wadau wa maendeleo USAID-MTaPS, kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO), Jukwaa la Afrika la Udhibiti wa Vifaa tiba, AUDA-NEPAD na TMDA.

Tunaishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Rais wetu Samia Suluhu Hassan pamoja na Wizara ya Afya kwa kutupatia uwezo ambao tunaonekana Bara la Afrika.’’ Amesema Bi. Kissa Mwamwitwa.

Ambapo amesema watabadilishana uzoefu ilikupata watalaam watakaokuwa wana uwezo wa kusaidia eneo hilo la vifaa tiba kwa akinamama na watoto kabla havijaingia sokoni.

“Ili kundi lilikuwa nyuma la akina mama, watoto wachanga na watoto wadogo. Hivyo kupitia mafunzo haya wadhibiti watakuwa wanatumika katika kutoa utalaam katika nchi zao baada ya kujifunza hapa.

Mafunzo haya yanafanyika kutokana na kuwa na mapungufu upande huo, na ni mara ya kwanza kufanyika hapa barani Afrika na tunashukuru Tanzania kuwa mwenyeji na pamoja na uwenyeji pia tumetoa watalaama ambao watashiriki kutoa mafunzo.’’ Amesema Bi. Kissa Mwamwitwa.

Wataalam hao wanatoka katika mamlaka za Udibiti wa vifaa tiba na vitendanishi kwa nchi za Afrika ikiwemo Uganda, Kenya, Ethiopia, Nigeria, Afrika Kusini, Botswana, Zambia, Rwanda, Ghana, Senegali na mwenyeji Tanzania.

Kwa upande wake Paulyne Wairimu ambaye ni Mwenyekiti wa Afrika Medical Forum-AMDF amebainisha kuwa Wadhibiti watapata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali ya tathimini na kufanyia kazi katika taasisi zao.

‘’Upande wa udhibiti vifaa vya Wamama na Watoto wachanga unaenda kupewa kipaumbele katika ukanda huu wa Afrika ilikusaidia eneo hili.’’ Amesema Paulyne Wairimu.

Nae mwakilishi kutoka USAID-MTaPs, Nereah Kisera amesema kuwa wanaendesha mpango wa vifaa kwa wamama na watoto kwa ufadhili chini ya USAID ambapo wakiwa na lengo la kuona kunakuwa na kujengewa uwezo mkubwa wa kuelewa juu ya vifaa upande wa udhibiti wa vifaa hivyo.

Mwisho.

YAWANOA WADHIBITI WA VIFAA TIBA BARANI AFRIKA JUU YA TATHMINI YA VIFAA TIBA VYA WAMAMA NA WATOTO

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba Nchini (TMDA) inaendesha mafunzo ya siku tatu Jijini Dar es Salaam ya kufanya tathmini ya udhibiti wa vifaa tiba vya Wamama, Watoto wachanga na Watoto kwa wataalam wa vifaa tiba kutoka Mamlaka za udhibiti za nchi 11 za Afrika.

Kongamano hilo ni la kwanza Barani Afrika ambapo mafunzo hayo yanafanyika kufuatia nchi za Afrika kutokuwa na uwezo wa kudhibiti bidhaa za Wakinamama na Watoto hivyo mafunzo hayo yatasaidia uwezo wa kutathimini bidhaa kabla hazijaingia kwenye soko.

Kongamano hilo la siku tatu, limezinduliwa mapema leo na Mkurugenzi wa Vifaa tiba na vitendanishi Kissa Mwamwitwa aliyekuwa amemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Adam Fimbo ambapo ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya kwa kuipa uwezo TMDA kujulikana Afrika na kuweza kutoa utaalamu ambao wanatoa kwa Nchi zingine.

“Warsha hii imedhaminiwa na Wadau wa maendeleo USAID-MTaPS, kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO), Jukwaa la Afrika la Udhibiti wa Vifaa tiba, AUDA-NEPAD na TMDA, Tunaishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Rais wetu Samia Suluhu Hassan pamoja na Wizara ya Afya kwa kutupatia uwezo ambao tunaonekana Bara la Afrika.’’

Amesema Kissa Mwamwitwa. Ambapo amesema watabadilishana uzoefu ilikupata watalaam watakaokuwa wana uwezo wa kusaidia eneo hilo la vifaa tiba kwa akinamama na watoto kabla havijaingia sokoni.

“Ili kundi lilikuwa nyuma la akina mama, watoto wachanga na watoto wadogo

. Hivyo kupitia mafunzo haya wadhibiti watakuwa wanatumika katika kutoa utalaam katika nchi zao baada ya kujifunza hapa. Mafunzo haya yanafanyika kutokana na kuwa na mapungufu upande huo, na ni mara ya kwanza kufanyika hapa barani Afrika na tunashukuru Tanzania kuwa mwenyeji na pamoja na uwenyeji pia tumetoa watalaama ambao watashiriki kutoa mafunzo.’’

Amesema Kissa Mwamwitwa. Wataalam hao wanatoka katika mamlaka za Udibiti wa vifaa tiba na vitendanishi kwa nchi za Afrika ikiwemo Uganda, Kenya, Ethiopia, Nigeria, Afrika Kusini, Botswana, Zambia, Rwanda, Ghana, Senegali na mwenyeji Tanzania.

Kwa upande wake Paulyne Wairimu ambaye ni Mwenyekiti wa Afrika Medical Forum-AMDF amebainisha kuwa Wadhibiti watapata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali ya tathimini na kufanyia kazi katika taasisi zao. ‘’Upande wa udhibiti vifaa vya Wamama na Watoto wachanga unaenda kupewa kipaumbele katika ukanda huu wa Afrika ilikusaidia eneo hili.’’ Amesema Paulyne Wairimu.

Nae mwakilishi kutoka USAID-MTaPs, Nereah Kisera amesema kuwa wanaendesha mpango wa vifaa kwa wamama na watoto kwa ufadhili chini ya USAID ambapo wakiwa na lengo la kuona kunakuwa na kujengewa uwezo mkubwa wa kuelewa juu ya vifaa upande wa udhibiti wa vifaa hivyo