May 17, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Taasisi ya Fahari watoa msaada wa vyakula kwa wanafunzi wenye Mahitaji maalum

Na Herishaban, TimesMajira Online, Ilala

TAASISI ya Fahari Tuamke Maendeleo iliyopo wilayani Ilala imetoa msaada wa vyakula na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa mahitaji Maalum wa shule ya Msingi Mzambarauni Jimbo la Ukonga .

Msaada huo ulitolewa na Mkurugenzi wa shule ya Fahari Day Care Neema Mchau ,kwa wanafunzi wa shule hiyo ili waweze kutumia kwani na wao ni sehemu ya jamii .

“Taasisi yetu ya Fahari imeweka utaratibu wake endelevu ambapo kila mwaka kutoa msaada kwa jamii ya mahitaji maalum misaada hii tunawashirisha Wazazi wa wanafunzi wa shule yetu “alisema Neema

Mkurugenzi wa Fahari Tuamke Maendeleo Neema Mchau ,alisema msaada huo waliotoa wa vyakula ni endelevu kila mwaka kusaidia jamii kwa kushirikiana na Wazazi wa wanafunzi wa watoto wanaosoma shule ya Fahari Day Care dhumuni kuwajengea upendo watoto wa mazingira magumu wakue katika msingi bora .

Alisema katika ziara hiyo shule ya msingi Mzambarauni wametoa vyakula mbali mbali ikiwemo mchele,sukari,maharage, unga na vifaa vya shule daftari ,peni sabuni ,Taulo za kike,

Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo iliyopo wilayani Ilala kata Gongolamboto inamiliki kituo cha watoto, wa Day Care ambapo ipo matari wa mbele kuunga mkono juhudi za Serikali katika sera ya elimu bure .

Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mzambarauni Maria Thomas Liyombo, alisema wanafunzi wa mahitaji maalum idadi yao 150 ambao wanasoma shule hiyo.

Mwalimu Maria Thomas Liyombo, alisema kila mwaka wanafunzi hao wa ,Kitengo maalum kitaaluma wanafanya vizuri katika masomo yao wameishauri Serikali kuongeza idadi ya walimu wa mahitaji Maalum.

Kwa upande wake Vivian Ugulumu kutoka (VIWOTA) alisema watoto viziwi wana uwezo wa kufanya mambo yote ambayo watoto wengine sio viziwi wanafanya hivyo ameishauri jamii kuongeza ulinzi kwa watoto wenye ulemavu sababu watu wengi utumia udhaifu wao.

Vivian alisema lengo kubwa la kuwajengea upendo na uwezo wawe wajasiri wa kuvunja ukimya pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia .

Alisema mtoto kiziwi anajengewa uwezo kwa ajili ya kuvunja ukimya akifanyiwa vitendo vya ukatili anakuwa na uwezo mkubwa kutoa ushahidi pindi anapofanyiwa vitendo vibaya.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo Neema Mchau akizungumza wakati wa kugawa chakula na vifaa vya shule katika shule ya Msingi mzambarauni iliopo Ukonga (Na Heri Shaaban )
Mkurugenzi wa shule ya Fahari Day Care Neema Mchau akikabidhi vyakula shule ya Msingi mzambarauni kwa Afisa Mtendaji wa kata
Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi mzambarauni Maria Thomas Liyombo akizungumza wakati wa kupokea msaada wa vyakula kwa wanafunzi wa Mahitaji maalum katika shule hiyo (Picha na Heri Shaaban)
Afisa maendeleo wa kata ya Ukonga