March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Regina Lubala,aungana na wananchi Pasiansi kupiga kura 

*Asisitiza wananchi kupiga kura

*Asema mazingira ni rafiki na usalama upo

Judith Ferdinand, Timesmajira Online-Mwanza 

Mgombe Udiwani wa Kata ya Pasiansi  kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),jimboni Ilemela mkoani Mwanza,Regina Lubala (PACOME),ameungana na wananchi wa  Kata hiyo katika zoezi la kupiga kura.

Ambapo leo Oktoba 29,2025, Tanzania inafanya uchaguzi mkuu wa kuchagua Rais,Wabunge na Madiwani,ambao wataongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Regina,ambaye ameungana na wananchi kupiga kura katika kituo cha Sunrise Sekondary A3,Kata ya Pasiansi.

Baada ya kupiga kura,Regina ametumia nafasi  hiyo kutoa wito kwa wananchi wa Kata ya Pasiansi na Tanzania kwa ujumla kujitokeza kupiga kura katika  vituo kwani mazingira  ni rafiki na hali ya usalama ni wa kutosha.