April 28, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Dkt. Samia ashiriki kilele cha sherehe za nanenane

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online, Mbeya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane ambayo Kitaifa yamefanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli pamoja na Dkt. Hussein Mohammed Omar Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo wakati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ugawaji wa vifaa vya maafisa ugani, trekta kwa wakulima, vifaa vya kutengeneza Vihenge vya chuma kwa Vijana, bei elekezi za mbolea ya ruzuku, mradi wa uchimbaji wa visima pamoja na ugawaji wa vifaa vya mfumo wa umwagiliaji kwa matone katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya Mkurugenzi wa Kampuni ya Asas Bw. Ahmed Salim kuhusu chakula cha Mifugo wakati alipotembelea Banda la Kampuni hiyo wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya mnufaika wa Mpango wa kuwawezesha Vijana kwenye Mifugo (BBT life Mifugo) Rest Mgonja kuhusiana na Mafanikio waliyopata kutokana na mradi huo wa ufugaji wa ng’ombe wa kisasa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Asas Bw. Ahmed Salim kuhusu ufugaji wa kisasa wa kondoo na mbuzi wa maziwa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo wakati alipotembelea vizimba vya kufugia Samaki katika moja ya mabanda ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapa chakula Samaki wanaofugwa kwenye vizimba wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Watoto wakati alipokuwa akipita kwenye mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera wakati akiangalia video fupi ya masuala ya Kilimo wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kuhusiana na ufugaji wa Samaki kwa Vijana katika vizimba kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.