May 17, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Philemon Kacheran apigwa marufuku
kutumia dawa za kusisimua misuli

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online

Mwanariadha wa Kenya wa mbio za marathon Philemon Kacheran Lokedi, amepigwa marufuku ya miaka mitatu baada ya kugundulika kutumia dawa iliyopigwa marufuku.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 alirejesha matokeo chanya ya “testosterone ya asili ya nje” katika jaribio lisilo la ushindani mwezi Aprili.

Kacheran aliondolewa katika timu ya Kenya kabla ya Michezo ya Jumuiya ya Madola mjini Birmingham, na anakuwa Mkenya wa tisa kupigwa marufuku na Kitengo cha Uadilifu cha Riadha (AIU) tangu mwanzoni mwa Julai.

Kipindi chake cha kutostahiki kimerejeshwa hadi tarehe 8 Julai, tarehe ya kusimamishwa kwake kwa muda.

Kacheran alikuwa amekabiliwa na marufuku ya miaka minne lakini alipunguziwa mwaka mmoja kwa sababu ya “kukiri mapema [hatia] na kukubali kuwekewa vikwazo”, imesema AIU.

Kacheran alimaliza wa nane katika mbio za Rotterdam Marathon mwezi Aprili, lakini alikimbia muda wake bora zaidi wa saa mbili dakika tano sekunde 19 alipomaliza wa tatu katika mbio za Valencia Marathon mwezi Desemba mwaka jana.