Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
Cristiano Ronaldo ameisababishia hasara ya mabilioni ya dola za Kimarekani kampuni inayotengeneza vinywaji vya Coca Cola baada ya kuondoa chupa za kinywaji hicho mbele yake wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
Kitendo hicho kilichosababisha hasara kiliadhiri hisa za kampuni hiyo kushuka kwa kiasi cha dola za Marekani Bilioni 4.
BOFYA CHINI KUTAZAMA VIDEO…
Kwa mujibu wa video iliyowekwa na mtandao wa gazeti la kila siku la Uingereza juzi(16/06/2021), The Guardian na kusambaa katika mitandao mbalimbali haswa ya jamii, ilimuonesha Ronaldo akiondoa chupa mbili za kinywaji cha Coca Cola mbele yake wakati akiwa katika mkutano na waandishi wa habari na kisha kuinua chupa ya maji na kusema kwa Kireno “kunywa maji, Coca Cola…”
Coca Cola ndio mdhamini mkuu wa mashindano ya Euro 2020, ilitoa tamko na kusema kila mtu ana uhuru wa kunywa kinywaji anachotaka, kwa mahitaji yake na mapenzi yake.
More Stories
AUWSA yazipatia maji kaya 6000 za kipato cha chini
Daraja la mto Kagatende Suluhisho la Kudumu Utalii na Uhifadhi Serengeti
Mkemia Mkuu:Tumedhibiti uingizaji na usafirishaji kemikali hatarishi nchini