Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online, Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Saidi Yakubu amekutana na na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Hamad Abdallah ambapo wamejadiliana namna kuendeleza ushirikiano baina ya pande mbili ili kuendeleza miundombinu ya michezo nchini.

Kikao hicho kimefanyika Juni 07, 2023 katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linatekeleza miradi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwemo jengo la ofisi za Wizara linalojengwa Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma pamoja na eneo la changamani la michezo Kawe jijini Dar es Salaam.
More Stories
Kapinga:Serikali inaboresha miundombinu ya umeme kibiti kuondoa changamoto ya umeme
Miaka 50 ya TET, waanza kupanda miti
Mwili wa Hayati Msuya wawasili Uwanja wa Ndege wa (KIA)