May 7, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Naibu Waziri Mkuu akutana na Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Bideko, amekutana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), CPA. Hosea Kashimba, Bungeni jijini Dodoma.

PSSSF, ni miongoni mwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

CPA. Kashimba alipata fursa ya kumpongeza Dkt. Biteko kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo Agosti 30, 2023 na kula kiapo Septemba 1, 2023.

Pia CPA. Kashimba alitumia fursa hiyo kujitambulisha ikiwa ni pamoja na kumueleza utekelzaji wa majukumu ya Mfuko kama yalivyoainishwa kwenye Sheria namba 2 ya mwaka 2018 iliyoanzisha PSSSF, ambayo ni pamoja na Kuandiskisha Wanachama, Kukusanya Michango, Kuwekeza na kulipa Mafao.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Bideko, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, ofisini kwa Naibu Waziri Mkuu kwenye ofisi za Bunge jijini Dodoma, Novemba 3, 2023. PSSSF iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Bideko (katikati), akipokea mfuko wenye taarifa mbalimbali kuhusu Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, ofisini kwa Naibu Waziri Mkuu kwenye ofisi za Bunge jijini Dodoma, Novemba 3, 2023. PSSSF iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kulia ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, PSSSF, Bw. James Mlowe.

Dkt. Bioteko (kulia), akiwa kwenye mazungumzo na ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na CPA. Kashimba. Wengine pichani ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, PSSSF, Bw. James Mlowe (wapili kushoto) na Afisa Mkuu wa Uhusiano, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi.