Meneja wa Serengeti Breweries mkoa wa Mwanza James Alphaxard, akizungumza na wateja wa vinywaji ya kampuni hiyo ya bia kwenye hafla ya makabidhiano ya zawadi iliyofanyika kwenye baa ya Makumbusho, kulia ni mshindi wa promosheni ya Maokoto ndani ya kizibo ambaye ni mkazi wa Igoma jijini Mwanza Melina Francis, ambapo alikabidhiwa mfano wa hundi ya Shilingi laki tano(5).Mshindi wa promosheni ya Maokoto ndani ya kizibo ambaye ni mkazi wa Igoma jijini Mwanza Melina Francis, akipokea mfano wa hundi ya Shilingi laki tano(5) kutoka kwa Meneja wa Serengeti Breweries mkoa wa Mwanza James Alphaxard (kushoto) kwenye hafla ya makabidhiano ya zawadi iliyofanyika kwenye baa ya Makumbusho.Mshindi wa promosheni ya Maokoto ndani ya kizibo ambaye ni mkazi wa Igoma jijini Mwanza Melina Francis, akionesha kwa furaha meseji ya muamala kwenye simu yake baada ya kutumiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Limited(SBL) kwenye hafla ya makabidhiano ya zawadi iliyofanyika kwenye baa ya Makumbusho.Wateja wa vinywaji vya Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Limited(SBL) wakituma namba za kushiriki promosheni ya Maokoto ndani ya kizibo eneo la Igoma jijini Mwanza, kwenye hafla ya makabidhiano ya zawadi ya mshindi wa promosheni hiyo iliyofanyika kwenye baa ya Makumbusho.
More Stories
Senyamule:Serikali inapaswa kuzitambua Kampuni zinazofanya biashara ya ardhi
Serikali kuendelea kupanua fursa elimu Singida
Kumekucha CDF Cup 2026, NMB yaweka Sh milioni 150