March 29, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mkurugenzi Paradise Mission apongeza serikali ya mkoa wa Mbeya

Na Esther Macha,Timesmajira,Online,Mbeya

SERIKALI mkoani Mbeya imepongezwa kwa kuendelea kuwajali wanawake katika shughuli mbalimbali ambazo wamekuwa wakifanya katika kijiinua kiuchumi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Paradise miision Pre&Primary School ,Ndele Mwaselela wakati akizungumza na wanawake wajasiliamali(Familia moja) kutoka kata mbalimbali Jijini hapa.

“Kupitia hadhara hii naomba nipongeze serikali ya mkoa chini ya mkuu wa mkoa wa mbeya Juma homera anafanya kazi kubwa ya kuwalea wanawake ,kwani nimeambiwa kila mnapotaka kufanya shughuli zenu mnapewa ukumbi bure pia ni mara chache sana kukuta baadhi ya mikoa wakifanya kitu kama hichi lakini mbeya imewezekana “amesema Mkurugenzi huyo .

Wanawake wajasiliamali wakimsikiliza mkurugenzi wa Paradise Mission Ndele Mwaselela