Na Mwandishi wetu,timesmajira,Online
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula leo amefungua Mafunzo ya Makatibu wa Mikoa Na Wilaya Nchi Nzima katika ukumbi wa Halmashauri Kuu wa Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma.
Pamoja na Mambo mengine ya msingi,Mangula amesema lengo la mafunzo hayo ni kujenga uelewa juu maadhumuni na imani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) sanjali na mambo mbalimbali ya ujenzi wa Taifa.
Aidha amesema mafunzo hayo yatafanyika kwa siku tatu kuanzia jana na zaidi ya mada 17 zitafundishwa na wakufunzi mbalimbali waandamizi wa Chama na Serikali.
Mafunzo hayo yatahitimishwa Novemba 6, 2021 ambapo Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufunga mafunzo haya.
More Stories
Prof.Muhongo achangia saruji mifuko 280,kuwezesha ujenzi wa zahanati 3
Serikali itaendelea kushirikiana na shule binafsi-Dkt. Biteko
Rais Mwinyi aumwagia sifa uongozi wa Samia