Na Mwandishi wetu,timesmajira,online
CHAMA cha Cha Mapinduzi CCM, kimepokea kwa masikitiko barua ya kujiuzulu kwa Mbunge Mteule wa CCM Jimbo la Konde, Sheha Mpemba Faki Leo Agosti 2,2021.
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,Itikadi na Uenezi CCM,Shaka Hamdu Shaka amesema katika barua yake, Sheha Mpemba Faki ameeleza kwamba amefikia uamuzi huo kutokana na changamoto za kifamilia, jambo ambalo Chama hakina uwezo wa kumzuia, hasa ikizingatiwa kwamba ni haki yake ya msingi kama ilivyo kwa haki ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ndani ya CCM.
Amesema Chama chao kinawaomba wanachama wote kuwa watulivu katika kipindi hiki wakati tukisubiri taratibu nyingine.
More Stories
Mfumo wa e-Board umeboresha uendeshaji vikao Ilemela
SOS Children’s Villages yawezesha ujenzi ofisi Dawati la Jinsia Nyamagana
Bil. 10/- za Samia zasomesha Madaktari Bingwa na Wabobezi wa saratani