March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mbaroni  tuhuma za kukutwa na viungo vidhaniwavyo vya binadamu

*Yumo mganga wa kienyeji, mfanyakazi wa mochwari 

Na Ashura Jumapili TimesMajira online Bukoba,

Jeshi la Polisi Mkoani Kagera linawashilikiwa watu  wawili  akiwemo mfanyakazi wa chumba cha kuhifadhi maiti(mochwari) hospitali ya Bwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe pamoja na mganga wa kienyeji, kwa tuhuma za kupatikana na viungo vinavyodhaniwa  kuwa vya binadamu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa  Kagera, Blasius Chatanda,amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Kelvin Mdollo( 42 )Mnyiha ambaye ni mganga wa kienyeji na mkazi wa Wilaya ya Mbozi  mkoani Songwe  pamoja na  Randani Mlomo mfanyakazi wa chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya Vwawa  iliyopo wilayani Mbozi mkoani  Songwe.

Chatanda,amesema, awali  Juni 17,2025,walimkata  Mdollo,akiwa na viungo vinavyodhaniwa  kuwa vya binadamu,ambavyo  ni mfupa mmoja wa taya inayowezekana kuwa ni ya  binadamu, kipande cha moyo wa binadamu,kipande cha sehemu ya siri ya mwanamke na  kipande cha kondo la nyuma la tumbo la uzazi la mwanamke.

Pia mtuhumiwa huyo  alikamatwa na vipande viwili vya ngozi  iliyokaushwa idhaniwayo kuwa ya nyoka aina ya chatu,ngozi moja ya nyoka wa kawaida,pembe mbili za mnyama wa porini,vipande vitatu vya mifupa ambayo bado haijatambulika kama ni ya mnyama au binadamu,ambavyo alikuwa akivitumia katika shughuli za uganga wa jadi na kupiga ramli chonganishi katika nyumba ya kulala wageni inayojulikana kama Standard iliyopo Kata ya Kibeta Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Amesema, baada ya mtuhumiwa wa kwanza ambaye ni mganga  kuhojiwa na polisi  alimtaja Randani  Mlomo ( 64 ) mfanyakazi wa hospitali ya Vwawa chumba cha kuhifadhia maiti iliyopo Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe,kwa madai kuwa  ndiye aliyempatia viungo hivyo.

Ambapo amesema  ndipo  jitihada  zilifanyika haraka ambazo zilifanikisha kumkamata Mlomo na kysafirisha hadi  mkoani Kagera,hivyo wanaendelea na mahojiano na watuhumiwa hao ili kubaini mtandao mzima unaojihusisha na matukio ya mauaji,ukataji wa viungo vya binadamu,uporaji pamoja na wanaojihusisha na kazi za uganga wa tiba  asili bila kuwa na vibali ikiwemo wanaopiga ramli chonganishi ili waweze kuchukuliwa hatua  kwa mujibu wa sheria za nchi.

Hata hivyo ametoa wito kwa wananch kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa kuhusu uhalifu na wahalifu huku akionya watu wote wanaojihusisha na shughuli za uganga wa jadi bila vibali kuacha mara moja akisisitiza  kuwa hatua  zitachukuliwa kwa watakaokamatwa.