Na Mwandishi wetu,timesmajira,Online
JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, linamshikilia mtu mmoja mwenye umri wa miaka 16 kwa madai ya kumlawiti mtoto wa miaka 4 na kusababisha kifo.
Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, ACP Muliro Muliro amesema jana kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 10, 2021 majira ya saa tatu asubuhi , Chamanzi Mbande Wilaya ya Temeke.
Amesema uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo unafanyika na hatua za kisheria wakati wa uchunguzi zitazingatiwa  ili itendeke pande zote mbili.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako