Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
WAZIRI wa Maji wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Profesa Makame Mbarawa amechukua fomu ya kuwania Urais wa Zanzibar.
Profesa Mbarawa amechukua fomu leo asubuhi katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui, ambako alikabidhiwa fomu na Katibu wa Oganaizesheni wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Galous Nyimbo.
Profesa Mbarawa ambaye pia amehudumu uwaziri katika Serikali ya Awamu ya Nne, anakuwa mwanachama wa 10 wa CCM kuchukua fomu tangu zoezi lilipoanza Jumatatu wiki hii

More Stories
BUWSSA yapokea bil.28.1 ya miradi,serikali awamu ya sita
STANBIC yaendelea kusaidia makampuni madogo ya uchimbaji mafuta na gesi
Mawakala kielelezo cha uwazi uboreshaji daftari la wapiga kura