Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
WAZIRI wa Maji wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Profesa Makame Mbarawa amechukua fomu ya kuwania Urais wa Zanzibar.
Profesa Mbarawa amechukua fomu leo asubuhi katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui, ambako alikabidhiwa fomu na Katibu wa Oganaizesheni wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Galous Nyimbo.
Profesa Mbarawa ambaye pia amehudumu uwaziri katika Serikali ya Awamu ya Nne, anakuwa mwanachama wa 10 wa CCM kuchukua fomu tangu zoezi lilipoanza Jumatatu wiki hii


More Stories
CCM yakemea vitendo vya ubakaji,ulawiti,ushoga
Dkt.Nchimbi atembelea Banda la REA
Ileje yatangaza kibano wasio na vyoo bora