
Na Mwandishi wetu, Timesmajira Online
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameonya dhidi ya kampeni zinazounga mkono haki za wapenzi wa jinsia moja nchini humo, Mapenzi ya jinsia moja ni haramu nchini Uganda.
“Usilete upuuzi wowote hapa, Tulikuwa Washington, na wakati huu Wamarekani walipanga mkutano vizuri kwa sababu hawakuleta masuala haya. Walijikita kwenye biashara, suala ambalo ni zuri. Hawakuleta masuala yeyote kuhusu wapenzi wa jinsia moja . Lakini kama wangeleta hizo mada tungekuwa na matatizo.” Rais Museveni
Ameyasema hayo Siku ya Jumatano Rais Museven alitaja haki za wapenzi wa jinsia moja kama “upuuzi” wakati wa hotuba aliyoitoa kwenye mahafali ya Chuo cha Kitaifa cha Ulinzi.

More Stories
TISEZA Songea kuvutia uwekezaji, ajira zaidi zapatikana
Serikali yajipanga kukabiliana na athari za El Nino
Wadau watakiwa kushirikiana Kuhifadhi Ziwa Tanganyika