Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline,Zanzibar
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Leo Jumapili Oktoba 8, 2023 amefika Langoni- Maungani, Wilaya ya Magharibi B Unguja, kwaajili ya Kuwafariji na Kutoa Mkono wa Pole kwa Wanafamilia wa Mzee Ismail Sharif, Kaka wa Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.

Hatua hiyo imekuja kufuatia Kifo cha Hasnuu Ismail Sharif (68), aliyefariki-dunia Usiku wa Kuamkia Jumamosi ya jana, hapo Nyumbani kwao Langoni-Maungani, baada ya kuugua kwa Majuma kadhaa.



Marehemu Hasnuu ambaye amewacha Mke na Watoto Watatu (3), pia amezikwa jana katika Makaburi ya hapo-hapo Langoni-Maungani, kisiwani Unguja.



More Stories
Wajenga nyumba ya watumishi kwa mapato ya ndani
Sangu: Michango ya Hifadhi ya Jamii ni Haki ya Msingi ya Mfanyakazi
Falsafa ya 4R Ya Rais Samia, yaongeza Ushirikiano wa Tanzania,China