Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline,Zanzibar
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Leo Jumapili Oktoba 8, 2023 amefika Langoni- Maungani, Wilaya ya Magharibi B Unguja, kwaajili ya Kuwafariji na Kutoa Mkono wa Pole kwa Wanafamilia wa Mzee Ismail Sharif, Kaka wa Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.

Hatua hiyo imekuja kufuatia Kifo cha Hasnuu Ismail Sharif (68), aliyefariki-dunia Usiku wa Kuamkia Jumamosi ya jana, hapo Nyumbani kwao Langoni-Maungani, baada ya kuugua kwa Majuma kadhaa.



Marehemu Hasnuu ambaye amewacha Mke na Watoto Watatu (3), pia amezikwa jana katika Makaburi ya hapo-hapo Langoni-Maungani, kisiwani Unguja.



More Stories
CCM yatoa salamu nzito kwa Samia-Butiama
Waziri wa Fedha aipa kongole CRDB
TAKUKURU Kinondoni yaainisha mafanikio Januari_ Machi 2016