Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Leo Februari 21, 2024 amefika na kutoa Mkono wa Pole kwa Familia ya Marehemu Mzee Kombo Ame, huko Garagara kwa Mbumbwini, Wilaya ya Magharib ‘A’ Unguja.
Marehemu Mzee Kombo ambaye ni Baba Mzazi wa Mmoja wa Wasaidizi wa Makamu, alifariki Dunia mapema usiku wa kuamkia juzi Februari 19, 2024 katika Hospitali ya Global, Mjini hapa.
Othman ambaye katika Ziara hiyo ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib, amewataka Wanafamilia kuwa na moyo wa subra katika kipindi hiki kigumu, sambamba na kuwataka kuzidisha Dua za Kumuombea Marehemu.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi, Amiin!
More Stories
TANAPA yapiga hodi Kagera kuelimisha Uhifadhi, Utalii
Maadhimisho siku ya nyuki Duniani ni fursa adhimu kiuchumi
NMB ‘yafunga ndoa’ na wanawake wanaomiliki shule, vyuo Tanzania