April 20, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Msanaa wa Hip hop Tupac Shakur enzi za uhai wake. (Picha na Mtandao).

Kwa taarifa yako: Marafiki walichanganya bangi na majivu ya Tupac na kuvuta

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online

MSANII wa muziki wa Hip hop Tupac Shakur aliyepata umaarufu mkubwa duniani na kupoteza maisha kwa kupigwa risasi katika ugomvi uliohusisha kurushiana risasi mwaka 1996 nchini Marekani katika jiji la Las Vegas, alikumbukwa na kundi aliloanzisha la Outlawz kwa kuchanganya majivu ya mwili wake na bangi na kisha kuvuta kama sigara.

Katika mahojiano na televisheni ya VladTV, kundi la The Outlawz walithibitisha uzushi uliokuwa ukisambaa kuwa kundi hilo lilichanganya majivu ya Tupac na bangi kisha kuvuta “smoked him out” kama heshima yao ya mwisho.

Kwa mujibu wa gazeti la The Independent la nchini Uingereza na https://www.huffpost.com/entry/outlawz-confirm-they-smoked-tupacs-ashes_n_942106, mmoja wa wasanii wa kundi hilo, Noble, alithibitisha kwa kusema, “Ndio ni kweli kabisa…tulikuwa katika kumbukumbu na familia yake pamoja na mama yake .

“Tulienda ufukweni na kutupa vitu vingi alivyovipenda baharini, kama bangi, vidari vya kuku, soda za chungwa. Pac alipenda vitu hivyo, sisi tuliamua kumuaga kwa mtindo huo,”alidai Noble

Naye EDI Mean kutoka bendi hiyo aliongeza kuwa, “Nilitoka na wazo hilo, kama ukisikiliza wimbo ya Tupac, ‘Black Jesus’ alisema ‘Ombi la mwisho, mvute majivu yangu.’ Hayo ndio matamanio yake, sijui alidhamiria kwa kiasi gani lakini sisi tumetekeleza”

Tukio hilo lilitokea katika kumbukumbu ya miaka 15 tokea kifo cha Tupac kilichotokea tarehe 13, Septemba 1996 ambapo marafiki na mashabiki wake walikutana katika kumbukumbu hiyo.

Kwa mujibu wa mtandao wa BET, marafiki zake wa muda mrefu wa Tupac Shakur, The Outlawz, wamedai kumkumbuka rafiki yao ambaye pia ndio mwanzilishi wa kundi hilo kwa namna ya pekee.

Katika sherehe hiyo baba yake Tupac alimkumbuka Tupac kwa kusema, “Tupac alithamini utu. Hilo ndio jambo kubwa, alijali sana watu kwakweli. Nafikiri ndio maana angekasirika sana iwapo watu wangejadili maamuzi yake katika kuwapenda watu weusi”.

Mtaalam wa masuala ya mifumo ya upumuaji, Dkt.Clifford Bassett kutoka jijini New York, Marekani akizungumzia juu ya hatua hiyo anasema,mtindo wa maisha ya kuiga na kuvuta vitu ambavyo havijaidhinishwa na wataalam wa afya ni hatari zaidi.

“Kuvuta kitu chochote ambacho hakijathibitishwa kutokana na aina yoyote ya vitu, hilo tunaliita kujitakia hatari usiyoijua. Mara nyingi huwa inaongeza athari na madhara makubwa katika mfumo wa upumuaji, hivyo ni hatari,”anasema.