Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Shirika la Umeme Tanzania TANESCO limeshinda tena tuzo kutoka Jamii Forums kwa utoaji majibu ya changamoto za wateja kwa wakati ,kuzifanyia kazi pamoja na utoaji wa taarifa mbalimbali.
Kupitia ukurasa hai (Thread ya TANESCO) inayoendeshwa kwenye Jukwaa la Jamii Forums, Tanesco wamekua wakijibu na kutoa suluhisho la matatizo mbalimbali ya wateja wanapopata changamoto za upatikanaji wa umeme Nchini.

Tuzo hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita zikihusisha taasisi mbalimbali za Serikali pamoja na Viongozi walio mstari wa mbele kwenye kutatua kero za Wananchi kupitia mitandao ya Kijamii kwa haraka kadri zinavyojitokeza.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako